Wednesday, July 18, 2012

TAARIFA YA KUZAMA KWA MELI  IKITOKEA DAR ES SALAAM KWENDA ZANZIBAR

Meli iliyokuwa imewabeba takriban watu miambili imethibitiswha kuzama katika bahari ya hindi eneo la Chumbe kisiwani Zanzibar. Meli hiyo kwa jina Star Gate ilikuwa inatoka Dar Es Salam kuelekea Zanzibar.
Kulingana na taarifa za vikosi vya wanamaji , meli hilyo ilianza kupata matatizo baada ya kutokea mawimbi makali.
Jeshi la polisi la wanamaji nchini Tanzania limeanza shughuli za kuwaokoa watu zaidi ya mbia mbili wanaohofiwa kuwa kwenye meli ya Skagit inayoripotiwa kuzama huko visiwani Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa za polisi, ingawa hawajathibitisha idadi kamili ya abiria waliomo kwenye meli hiyo, lakini wamethibitisha kwamba meli hiyo imepigwa na dharuba ya upepo mkali katika eneo la Chumbeambalo ni umbali wa kilometa 13.8 kutoka bandari ya Zanzibar  pindi ilipokuwa inatoka jijini Dar es Salaam kuelekea visiwani Zanzibar.


 

                                          

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                        

Tuesday, July 17, 2012


TUNAWEZA KUTIBU KIINI CHA TATIZO SEKTA YA NISHATI YA UMEME

 

Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika
Kwa nafasi ya Uwaziri Kivuli wa Nishati na Madini, nafahamu kuna ufisadi na ubadhilifu ndani ya TANESCO ambao uchunguzi ni muhimu kwa ajili ya uwajibikaji. Kusimamishwa kwa Mkurugenzi wa TANESCO na maafisa wengine wa shirika hilo kupisha uchunguzi ni muhimu, lakini si muarubaini wa uozo wa kimfumo katika sekta ya nishati nchini nitatoa vielelezo vya kina wakati nitakapo wasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni katika wizara ya Nishati na Madini.
Hata hivyo ni vyema nikatahadharisha mapema kuwa tukio hili linapaswa kutafakariwa kwa upana kwa kuwa linahusisha masuala mengi ambayo mengine Bodi ya Wakurugenzi imeyaacha nyuma ya pazia. Ukweli wote utakapotoka hadharani wengine zaidi watapaswa kuwajibika au kuwajibishwa kwa maslahi ya Taifa!
Kwa nyakati mbalimbali toka mpango wa dharura wa umeme uwasilishwe bungeni, nimekuwa nikiitahadhalisha na kuihoji serikali (kama sehemu ya jukumu langu la kibunge) kwa uzembe, ufisadi na udhaifu wa kiutendaji katika serikali ambao hasara yake utairejesha nchi katika mgao wa umeme hali ambayo imedhihirika hivi sasa!
Kusimamishwa kwa Mkurugenzi wa Tanesco na watendaji wake ni kafara ya kuficha uzembe na udhaifu wa serikali kwa ujumla wake kwa kuwa taarifa za utendaji wa Tanesco kuhusu mpango wa dharura wa umeme zimekuwa zikijadiliwa kwenye vikao vya wizara ya nishati na madini na hata vikao vya baraza la mawaziri bila hatua muafaka kuchukuliwa. Ninazo nyaraka za ndani za serikali na taasisi zake. Iwapo serikali haitatoa kauli bungeni ni kwa nini Waziri wa Nishati na Naibu wake anayehusika na Nishati kutoa taarifa potofu bungeni kuwa hakuna mgao wa umeme, aidha waeleze mkakati dhaifu waliokuwa wakiufanya kupunguza mgao katika kipindi cha bunge ili kuficha udhaifu na uzembe uliokithiri serikalini na katika wizara mahsusi!

Mazishi ya Watu walio kufa kwa GONGO Dar


Huu ndo ukweli kamili kuhusu vifo vya watu sita waliokunywa gongo Kigogo Sambusa Luhanga Darajani, ambapo wengine wamelazwa wakiwa hoi katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam umebainika.
Gazeti hili limegundua kuwa gongo waliyokunywa ilikuwa ina mchanganyiko wa kemikali mbalimbali na dawa za viwandani na tayari sampuli yake imepelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali kwa uchunguzi zaidi.
Mteja mmoja ambaye kwa kipindi cha nyuma alikuwa ‘mnywaji mzuri’ wa gongo katika eneo hilo ambaye hakutaka atajwe gazetini alichambua jinsi pombe hiyo inavyotengenezwa.
Alisema kuwa kuna kemikali zinozotumika kutengezea konyagi ambapo watengenezaji wanazipata katika kiwanda kimoja (jina tunahifadhi) na wanachanganya na dawa nyingine.
Alibainisha kuwa kemikali moja hujazwa kwenye chupa ya ujazo wa lita moja na kuchanganywa na maji kiasi cha lita kumi kisha hutiwa spiriti pamoja na dawa ya madoa iitwayo ‘jick’ na mchanganyiko huo huzalisha kitu kinachoitwa gongo na kuanza kusambaziwa wateja.
Chanzo hicho kilisema kuwa njia hiyo ndiyo aliyokuwa akiitumia Hekima Bakari kwa muda mrefu, mama anayedaiwa kuwauzia gongo watu waliofariki na kulazwa Hospitali ya Amana.
Kiliendelelea kufafanua kuwa mama huyo ametengeneza mtandao na alikuwa akisambaza kinywaji hicho Gongo la Mboto, Kipunguni, Chanika, Kitunda, Kimara Bucha na Kigamboni.
Gongo hiyo ilianza kuua Jumatatu ya wiki iliyopita ambapo ilimuua Juma Abdallah baada ya kunywa kinywaji hicho na wanywaji wengine wakawa wanajificha kwa kuwa walikuwa wakiogopa kukamatwa na polisi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa serikali ya mtaa katika eneo hilo la Kigogo Mbuyuni, Mohammed Mnunga aliwataka wote waliokunywa gongo hiyo kujitokeza na kwenda kupimwa afya zao kwa usalama wao.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Charles Kenyela amepiga marufuku mtu yeyote kujihusisha na kupika, kuuza au kunywa pombe haramu ya gongo na akasema tayari watu kadhaa wamekamatwa kuhusiana na sakata hilo.
Aliwataja watuhumiwa waliokamatwa hadi sasa kuwa ni Ramadhan Selestin (30), Salehe Omary (17), Shukuru Marungu (20), Charles Ibrahim (20), Fadhili Juma (20) wote ni wakazi wa Kigogo na Abdallah Mnazi (30) mkazi wa Tabata.
Aliwataja pia waliofariki katika nyakati tofauti kuanzia Julai 7 hadi 12, mwaka huu, katika maeneo ya Kigogo Mbuyuni kuwa ni Juma Abdallah (60), Mathew Roman (35), Khalid Hamis (31), Mohamed Said (25) na Antipal Raphel (60) wote wa Kigogo Mbuyuni na Hekima Bakari, ambaye ni muuzaji wa gongo hiyo.

 

Thursday, June 28, 2012

YALIYOMSIBU DR.STEVEN ULIMBOKA

YALIYOMSIBU  DR.STEVEN ULIMBOKA

Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova amezungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo la utekaji nyara na kujeruhi lililompata kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka anayedaiwa kutekwa na watu watano wakati akipata kinywaji katika klabu ya Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.
Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezi kuwa msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka katika msitu wa Mabwepande na kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo
MENGINE 
 Akisimulia mkasa huo mmoja wa madaktari wenzie aliyefahamika kwa jina moja la Dkt Deo, alisema kuwa alipigiwa simu na mtu hasiyemfahamu na kumfahamisha tukio hilo.




Alisema alipofika katika kituo cha Polisi cha Bunju, alimkuta akiwa katika hali mbaya na ilikuwa ngumu kumtambua kwakuwa alikuwa na majeraha mengi eneo la usoni.


Aliongeza kuwa akiwa na wenzie waliamua kumchukua na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwaajili ya matibabu.

 
Gari iliyokuwa imembeba Dr.Steven Ulimbika ikisukumwa na Wauguzi na Madaktari Hospitalini Muimbili