Thursday, June 28, 2012

YALIYOMSIBU DR.STEVEN ULIMBOKA

YALIYOMSIBU  DR.STEVEN ULIMBOKA

Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova amezungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo la utekaji nyara na kujeruhi lililompata kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka anayedaiwa kutekwa na watu watano wakati akipata kinywaji katika klabu ya Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.
Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezi kuwa msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka katika msitu wa Mabwepande na kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo
MENGINE 
 Akisimulia mkasa huo mmoja wa madaktari wenzie aliyefahamika kwa jina moja la Dkt Deo, alisema kuwa alipigiwa simu na mtu hasiyemfahamu na kumfahamisha tukio hilo.




Alisema alipofika katika kituo cha Polisi cha Bunju, alimkuta akiwa katika hali mbaya na ilikuwa ngumu kumtambua kwakuwa alikuwa na majeraha mengi eneo la usoni.


Aliongeza kuwa akiwa na wenzie waliamua kumchukua na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwaajili ya matibabu.

 
Gari iliyokuwa imembeba Dr.Steven Ulimbika ikisukumwa na Wauguzi na Madaktari Hospitalini Muimbili

Sunday, June 24, 2012

MJENGONI BIG BROTHER STAR GAME NEWS

MSHIRIKI KUTOKA SOUTH AFRICA BABZ KUTOLEWA (EVICTED)

Siku ya 49 ya msimu wa 7 BBA Star game mshiriki kutoka South Afrika BABZ kutolewa nje ya mashindano hayo akitokea jengo la Upvile kulikokuwa na mchuano wa kutoana jumatatu waliochaguana kwa ajili ya kutoana ni Babz kutoka (SA) Maneta (ZIM) na Prezzo (KE) kutokana na nguvu kutoka kwa kiongozi wa nyumba wa wiki  Mshiriki Gold kutoka Nigeria kuamua  kumtoa Prezzo mtuwake wake wakaribu katika kinyang'anyiro cha kutolewa badala ya Babz na kumweka kijana Keita kutoka Ghana kwenye kinyanganyiro cha kutolewa akielezea kwa masikitiko makubwa kiongozi wa wiki iliyopita kuwa aliamua kumtoa Prezzo kwenye kinyang'anyiro cha kutoka ni kutokana walipeana ahadi ya kutosalitiana kipindi chote watakacho kuwa mjengoni hapo na kumwomba msamaha rafiki yake Babz msamaha kwa maamuzi aliyochukua uku kijana keita kupokea taarifa hiyo na kuamua kwenda kuweka nguo sawa kabla ya maamuzi kutoka mshiriki Maneta na mwenzake Roki  kutoka zimbabwe walitolewa mapema wiki hii kwa kuvunja masharti kwa kutaka kupigana na kutoheshimiana huku jumba la down vile  walikokuwa wamebaki couple nne  na  mbili zenye hatihati ya kutoka ni kundi la Malawi na Zambia wanaweza wawili wakabaki katika hayo makundi kwenda kuungana na wenzao wa up vile kutoka Malawi ni vijana Nafe na Wati na kutoka Zambia ni Mabinti Tamara na Talia






BABZ

Babz baada ya kutolewa







Babz na Keita


Vimpira nomination wiki hii

Prezzo na Gold